Tanzania
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, Profesa Kitila Mkumbo, amefafanua kuwa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025 - 2050 ina jumla ya shabaha 18, ambapo shabaha kuu ni kwa Tanzania kuwa na Pato la Taifa lenye thamani ya dola trilioni moja za Kimarekani na wastani wa pato la mtu mmoja lenye thamani ya dola elfu saba kwa mwaka ifikapo mwaka 2050.
Julai 17, 2025